Kongani ya Bagamoyo imeendelea kuwa kitovu cha uwekezaji nchini baada ya kupokea maombi 48 kati ya maombi 86 yaliyowasilishwa TISEZA hadi kufikia Aprili Mosi mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gilead Teri, amesema mwitikio huo unaonyesha imani kubwa ya wawekezaji katika eneo hilo.
Amesema mbali na Bagamoyo, kongani ya Kwale imepokea miradi 20, huku Nala na Buzwagi zikibaki na miradi miwili kila moja.
Kwa mujibu wa Teri, mafanikio hayo yanachangiwa na uwepo wa miundombinu bora pamoja na sera rafiki za uwekezaji zinazotekelezwa na Serikali.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo













