Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 13 Novemba, 2020 amefanya uteuzi wa Mawaziri wawili katika Baraza jipya la Mawaziri, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya ndugu, Gerson Msigwa ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU leo Novemba 13, 2020 katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Amesema,Rais Magufuli amemteua Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Pili, Rais Magufuli amemteua Dkt. Philip Isdor Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango. Mawaziri Wateule hao walikuwa wakishikilia nyadhifa hizo katika Baraza la Mawaziri lililopita na uteuzi huu unaanza leo tarehe 13 Novemba, 2020.
Amesema,Rais Magufuli amemteua Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Pili, Rais Magufuli amemteua Dkt. Philip Isdor Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango. Mawaziri Wateule hao walikuwa wakishikilia nyadhifa hizo katika Baraza la Mawaziri lililopita na uteuzi huu unaanza leo tarehe 13 Novemba, 2020.
Tags
Habari