Kafulila: Sijaja kutengua, nimekuja kutimiliza

Na Derick Milton, Simiyu

Mkuu wa mkoa mpya wa Simiyu David Kafulila amesema kuwa, atahakikisha anaendeleza yale yote mazuri hasa upande wa Elimu ambayo yalianzishwa na mtangulizi wake ambaye alikuwa Mkuu wa mkoa huo sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka.

RC Mtaka akimkabidhi ofisi RC Kafulila
Kafulila amesema hayo leo, wakati wa hafla ya kukabidhiwa ofisi, ambapo amesema kuwa kuteuliwa kwake kuwa mkuu wa mkoa huo siyo kwa ajili ua kuja kutengua bali kwa ajili ya kutimiliza.

Amesema kuwa mkoa wa Simiyu umefanya vizuri katika sekta ya elimu chini ya Anthony Mtaka, na kubainisha kuwa atahakikisha anaendeleza pale ambapo Mtaka ameacha na kufika mbele zaidi.

Aidha Mkuu huyo wa mkoa, ameomba ushirikiano mkubwa kutoka kwa viongozi mbalimbali wa mkoa huo, ili kuhakikisha wanafikia malengo makubwa ambayo mkoa umejiwekea na kuwaletea Maendeleo wananchi.

"Mkoa wa Simiyu unaso raslimali nyingi kama mifugo, kilimo, Madini, Jambo ambalo amesema ni fursa kubwa kwa wananchi wa mkoa huo kuzitumia na kuweza kujiletea Maendeleo," amesema Kafulila.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Tabora Anthony Mtaka akizungumza katika hafla, aliwashukuru watendaji wote wa serikali, viongozi, na wananchi kwa ushirikiano ambao walimpatia na kufikia malengo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news