Na CATHERINE MBIGILI,Iringa
Akizungumza wakati wa utambulisho katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkuu huyo alisema kuna ulazima wa kuisadia timu hiyo kuendelea kubaki licha ya kusalia siku chache ili kucheza mchezo wake wa mwisho.
"Siku zinaonekana zimeisha, lakini siku moja Inaweza kuwa kubwa na ikaleta mabadiliko makubwa na timu ikafanya vizuri,"amesema Queen.
Alisema, hali ya timu ni mbaya baada ya kushuka ligi kuu lakini haifanyi vizuri hivyo imebakiza mechi moja ambayo wanakwenda kuicheza Jumamosi.Katibu huyo aliomba kabla ya mechi hiyo kuchezwa kama viongozi wakutane na uongozi wa timu ili kuona kitu gani cha kufanya ili kuisaidia timu kusalia.
Alisema, endapo wangeisaidia mwakani ingerudi ligi kuu na kusaidia vijana kupata ajira na kukuza uchumi wa wana Iringa.
Alisema, watu wa Iringa hawachukulii michezo kama ni ajira na hivyo kutoitilia umakini na msisitizo kama ilivyo kwa mikoa mingine.
"Timu kama Yanga na Simba zinapokuja hapa kwetu zinatumia gharama ambazo wananchi wa Iringa wanajipatia kipato kwa vijana pamoja na wafanyabiashara,"amesema Katibu.

