TAGCO WAMPA TUZO DKT.ABBASI KUTAMBUA MCHANGO WAKE

Na John Mapepele, Mbeya

Katibu Mkuu wa Habari wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi ametunukiwa tuzo na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) kwa kutambua mchango na mageuzi makubwa aliyoyafanya kwenye Sekta ya Habari hapa nchini. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi, akitunukiwa Tuzo ya Shukrani kutoka kwa viongozi na wanachama wa Chama cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) kwa mchango wake aliotukuka kwenye kuleta mageuzi katika sekta ya habari nchini.

Akikabidhi tuzo hiyo kwa Dkt. Hassan Abbasi, Mwenyekiti wa TAGCO, Paschal Shelutete wakati wa kikao cha 16 cha TAGCO kilichofanyika Jijini Mbeya Mei 24,2021 amesema Dkt. Abbasi ametoa mchango mkubwa akiwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Mkuu wa Serikali tofauti na hapo awali.

“Ni katika kipindi hiki ambapo miradi ya kimkakati ya Serikali ilisemewa vizuri zaidi na kufahamika na watu wengi hivyo kuwafanya wananchi kuipenda Serikali yao” Amefafanua Shelutete.

Ameongeza kwamba Dkt. Abbasi amefanikiwa kusimamia tasnia ya Habari na uboresha mahusiano ya kikazi miongoni mwa wadau wote wa Sekta ya Habari.

kwa upande wake Dkt. Abbasi amewashukuru Waandishi kwa kumpa tuzo hiyo na kuahidi kuendelea kuwapa ushirikiano ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu wao kikamilifu kwa nafasi yake ya sasa ya Katibu Mkuu. Wizara ya Habari, Utamadunim Sanaa na Michezo.

“Tuendelee kushirikiana katika cheo hiki kipya cha Katibu Mkuu katika Wizara yetu ambayo ni Wizara muhimu inayogusa umma kwa nyanja ya burudani na huzuni kutokana na Sekta zake Ameongeza Dkt. Abbasi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi (katikati) akiongoza kikao kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini Jijini Mbeya, kushoto ni Naibu wake Dkt. Ally Possi, kulia ni Katibu Mkuu -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe.

Amewataka Waandishi kuzingatia weledi wakati wote wa undaji wao wa kazi ambapo amesisitiza kwamba Serikali inatambua mchango wa waandishi na kwamba itaendelea kuhakikisha sekta inaboreka na kuchangia kwenye uchumi wa Taifa.

Aidha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumwamini na kumrejesha tena kwenye nafasi ya Katibu Mkuu na kuahidi kufanya kazi kwa weledi na bidi ili kutekelea Ilani ya Chama cha Mapinduzi na maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia.

Kikao hiki kimefunguliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa kimehudhuriwa na Naibu wa Wizara hiyo, Katibu Mkuu -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe ambaye ametoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kiutumishi kwa maafisa Habari kutoka halmashauri zote nchini,na viongozi mbalimbali wa Serikali na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali zaidi ya 270.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news