Ziara ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii mkoani Lindi


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Mary Masanja (Mb) akimsikiliza Mhifadhi Mkuu, Hifadhi ya Mazingira Asilia Rondo, Richard Baltazar (kulia) akitoa maelezo kuhusu Hifadhi ya Mazingira Asilia Rondo alipokuwa akikagua shamba la miti Rondo katika ziara yake ya kikazi jana Mkoani Lindi. Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Mary Masanja (Mb) akimwagilia mti wa kumbukumbu alioupanda wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Huduma za Miti (TFS) Shamba la Miti Rondo Mkoani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Kanda ya Kusini wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Manyisye Mpokigwe Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Mhe. Mary Masanja (Mb) akizungumza na wanachi wa Kijiji cha Rondo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi katika ziara yake ya kikazi ya kusikiliza kero za wananchi ambapo amewataka wananchi kuendelea kuhifadhi mazingira ili kuendeleza utalii wa eneo hilo Mkoani Lindi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news