Wanafunzi waliotekwa nyara na kuachiwa huru waungana na familia zao

ABUJA, Wanafunzi 15 wameungana tena na familia zao wiki saba baada ya kutekwa nyara kutoka shule yao iliyopo Kaskazini Magharibi mwa Nigeria. Mwanafunzi aliyekuwa ametekwa na kuachiwa huru akiungana na familia yake katika Shule ya Sekondari ya Bethel Baptist huko Damishi nchini Nigeria. (Picha na AP).

Kwa mujibu wa VOA, mzazi mmoja anasema, baadhi ya wanafunzi hao wako hospitali kwa matibabu baada ya kukumbwa na madhila hayo.

Kwa ujumla wanafunzi 121 walitekwa nyara kutoka shule ya sekondari ya Bethel Baptist katika jimbo la Kaduna na polisi wanasema juhudi zinaendelea kuwatafuta wanafunzi 65 ambao bado wanashikiliwa.

Kiongozi mmoja wa mji anasema, fidia imetolewa ili kuachiliwa kwa wanafunzi lakini watekaji nyara wamewaachilia wachache kuliko idadi walioahidi.

Maafisa wa usalama wa Nigeria wameshiundwa kuzuia utekaji wa halaiki unaonedelea nchini humo zaidi ya wanafunzi elfu moja wameshatekwa tangu Desemba, mwaka jana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news