Wanawake wazidi kupaisha soka la Tanzania, CECAFA Challenge Women’s 20 waanza kwa ushindi

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Clara Luvanga dakika ya 90 ameongeza furaha kwa Watanzania baada ya kuiwezesha timu ya Tanzania kusonga mbele.
Ni kupitia michuano ya wasichana chini ya umri wa miaka 20 Afrika Mashariki na Kati (CECAFA Challenge Women’s 20) baada ya kuichapa Eritrea 1-0 jioni ya leo Uwanja wa FTC Njeru nchini Uganda.

Kwa ushindi huo, timu hiyo itashuka tena dimbani Jumatatu kumenyana na Burudani kabla ya kuivaa Ethiopia Jumatano, Uganda Jumamosi ijayo na kukamilisha mechi zake kwa kucheza na Djibouti Novemba 9, mwaka huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news