Kigoma wagoma kulipia bili za maji kwa madai yanaletwa na Mungu

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Baadhi ya wakazi wa Wilaya ya Kigoma mkoani Kigoma wameripotiwa kugoma kulipia huduma ya maji kwa kile wanachodai kuwa bidhaa hiyo inaletwa na Mungu.

Akizungumza katika mkutano wa nusu mwaka wa Wakala wa Usabazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani Kigoma, Meneja wa wakala huo wilayani humo, Mhandisi Leo Respicius amesema, tabia hiyo imechangia kupungua kwa mapato yanayotokana na huduma ya maji katika baadhi ya vijiji.

Aidha, kutokana na changamoto hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Ester Mahawe ameitaka RUWASA kushirikiana na viongozi wa vijiji wilayani humo ili kuwaelimisha zaidi wananchi juu ya umuhimu wa kulipia huduma ya maji.
Vijiji vya Mkongoro, Kaseke, Nyamoli na Kidahawe ndipo ambapo baadhi ya wakazi wake wanadaiwa kugoma kulipia huduma hiyo kwa madai maji yameletwa na Mungu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news