Magazeti leo Agosti 18,2026

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeteketeza tani 39 za bidhaa za chakula zisizokidhi matakwa ya viwango, zenye thamani ya takribani Sh milioni 149, ikiwa ni hatua ya kuwalinda wananchi dhidi ya matumizi ya bidhaa zisizo salama.
Zoezi hilo limefanyika Agosti 17, 2026, katika eneo la Mbezi Gongoni, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, baada ya bidhaa hizo kubainika kuwa na mapungufu mbalimbali wakati wa ukaguzi wa mara kwa mara uliofanywa na TBS kati ya Julai na Agosti mwaka huu.

Meneja wa TBS Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji, amesema ukaguzi huo umebaini baadhi ya bidhaa za chakula zikikosa alama ya ubora pamoja na taarifa muhimu kwenye vifungashio, hali inayoweza kuhatarisha afya za watumiaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here