Moto wateketeza hoteli za kitalii Zanzibar ikiwemo Villa de Coco ya Jambiani

NA MWANDISHI MAALUM

MOTO ulioanzia jikoni katika Hoteli ya Villa de Coco iliyopo Jambiani jijini Zanzibar umeteketeza hoteli tatu na kuunguza vyumba vingine sita vya hoteli jirani ya nne.

Ni kutokana na upepo mkali wa baharini na zana chache za kuzimia moto usiku wa Novemba 19,2021.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Suleiman Hassan amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema hakuna mtu yeyote aliyedhurika wakiwemo wageni wa hoteli hiyo pamoja na wamiliki wa hoteli.
Kwa miaka kadhaa sasa, matukio ya ajali z moto yamekuwa yakizikabili hoteli mbalimbali za Kitalii jijini Zanzibar.
DIRAMAKINI Blog tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kadri zitakavyotufikia katika chumba chetu cha habari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news