RC Kafulila kuzifumua AMCOS Simiyu

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mheshimiwa David Kafulila leo Novemba 10,2021 amemwelekeza Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Simiyu, Joshua Msuya kukagua malipo yote ya AMCOS.

Ameyasema hayo wakati akihutubia Baraza la Madiwani Wilaya ya Maswa mkoani hapa huku akisisitiza kuwa, hatua za haraka zitachukuliwa ili kumneemesha mkulima na si kumdidimiza.
Amesema, lengo ni kubaini AMCOS zote zilizoshirikiana na maafisa ushirika kukiuka taratibu za malipo ya fedha, wenyeviti na makatibu wake sambamba na maofisa ushirika watakaobainika kushiriki mchezo mchafu huo waweze kuwajibishwa.

Pia Kafulila amewataka wakulima wote wa Pamba kujiunga na ushirika kwani atahakikisha kuwa anaondoa virusi wote kuanzia maofisa ushirika halmashauri mpaka viongozi wa AMCOS.

"Lengo ni kuhakikisha Serikali kwa kushirikia na ushirika tunamkomboa mkulima mdogo, na hilo lengo litafikiwa kama ilivyokuwa miongo kadhaa baada ya Uhuru,"amesema RC Kafulila.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news