SERIKALI KUONDOA ZUIO LA BIASHARA YA USAFIRISHAJI WANYAMAPORI HAI NJE YA NCHI

NA HAPPINESS SHAYO-WMU

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema Serikali itaondoa zuio la biashara ya usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi lakini wafanyabiashara watatakiwa kuzingatia taratibu za usafirishaji.
Ameyasema hayo leo bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Eng. Mwanaisha Ulenge aliyehoji lini Serikali itaruhusu usafirishaji wa viumbe hai nje ya nchi.

Mhe. Masanja amefafanua kuwa baada ya Serikali kutathmini kuhusu usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi imekubali kuondoa zuio hilo kwa masharti kwamba wanyamapori hai wasafirishwe kwa shughuli za utafiti na kidiplomasia tu; wawe wamekaushwa au ni mazao yatokanayo na wanyamapori na kwamba wasafirishaji hao ni lazima wawe ni wafanyabiashara wenye miradi ya ufugaji wanyamapori ili kuhamasisha uanzishwaji wa miradi ya ufugaji wa wanyamapori.

Aidha, Serikali itatoa muda wa miezi mitatu kuruhusu wafanyabiashara kusafirisha wanyamapori waliosalia kwenye mazizi na mashamba kabla ya zuio ambao walikuwa wanafugwa kwa lengo la kuwasafirisha nje ya nchi.

Serikali ilisitisha biashara ya kusafirisha wanyamapori nje ya nchi tartehe 17/03/2016 baada ya kuonyesha matokeo hasi ya biashara ikiwa ni pamoja na uhamishaji warasilimali za wanyamapori nje ya nchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news