Tazama Daraja la Mto Ruhuhu lilivyorejesha faraja kwa wananchi

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

MSEMAJI Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Gerson Msigwa amekumbushia moja wapo ya kumbukumbu muhimu katika maisha yake wakati akitekeleza majukumu yake kama mwanahabari mwaka 2013.

"Nimekumbuka mwaka 2013. Hapo ilikuwa tunavuka Mto Ruhuhu ambao ni mpaka wa Wilaya ya Nyasa (Ruvuma) na Ludewa (Njombe).

"Kuvuka hapo ilikuwa lazima Wazee wajulishwe. Yaani hapo nipo kwenye mtumbi nampiga picha Nape Nnauye na ng’ambo ya pili Mzee Abdulrahaman Kinana anaangalia vijana watavuka kweli?.

Mzee Kinana mwenye alivuka kikakamavu mno huku anapiga saluti. Mnaokumbuka ilikuwa ni Operesheni nini vile?.
Mzee Kinana wakati huo alikuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa
huku Nape Nnauye ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Jimbo la Mtama mkoani Lindi akiwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news