WAZIRI UMMY MWALIMU AWAPONGEZA VIONGOZI HALMASHAURI YA TEMEKE

NA MWANDISHI MAALUM

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Ummy Mwalimu amewapongeza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke, akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mkurugenzi pamoja na watumishi kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya katika kusimamia miradi ya maendeleo.
Ametoa kauli hiyo leo Novemba 15,2021 wakati wa ziara yake ya kutembelea na kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia, kupitia Miradi ya Kimkakati ya Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Miradi hiyo ambayo ilikuwa kwenye awamu ya kwanza ya utekelezwaji wake, kwa sasa imekamilika na imekua chachu kubwa ya maendeleo na faida kwa Wananchi,huku zaidi ya bilioni 650 zikiwa zimetumika katika utekelezwaji wake kwa manispaa ya Temeke.
Waziri Ummy alibainisha kwamba kupitia fedha za Benki ya Dunia, katika kuboresha huduma za jamii,miundombinu ya Dar es Salaam ikiwemo kujenga barabara,vituo vya afya na masoko,maeneo mengi katika jiji yamebadilika na kupendeza.

Aidha, amewashukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano huo,mbali na shukrani hizo, amewaomba kwamba katika awamu zijazo,waongeze ushirikiano katika kuboresha maeneo mengine ambayo bado hayajafikiwa na mradi huo.
Katika ziara hiyo Ummy amewangozana na viongozi mbalimbali wa Benki ya Dunia akiwemo Mari Pangestu ambaye ni mkurugenzi wa sera, maendeleo na ushirikiano wa benki hiyo. Kwa pamoja walitembelea soko la Makangarawe na kituo cha afya Buza.

"Sekta ya afya imeimarika, vituo vipo vizuri, visafi, lakini tangu kituo hicho kimeanza kutoa huduma, hawajapata kifo kinachotokana na ujauzito au uzazi, kwa hilo amewapongeza sana,"amesema Waziri Ummy.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news