Kocha Mkuu wa El-Magd SC afariki kwa mshtuko baada ya ushindi usiotarajiwa

NA GODFREY NNKO

MCHEZAJI wa zamani wa Ismaily na Kocha Mkuu wa Timu ya Al Magd inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini Misri, Adham El Selhedar amefariki dunia baada ya timu yake kumaliza mchezo dhidi ya Al Zarka.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Desemba 2, 2021 katika dimba la Alexandria, Cairo nchini Misri wakati wakali hao wakiumana ambapo walipiga dakika tisi wakiwa na matokeo tasa.

El-Magd ya Alexandria walikuwa wanachuana na Al-Zarka katika siku ya tisa ya msimu wa mchezo ulionekana kuelekea sare tasa.

Vijana hao wa Alexandria, hata hivyo, walifanikiwa kupata bao la ushindi katika dakika ya 92 kupitia Mohamed Saad na kufanikiwa kupata alama tatu.

Wakati wa sherehe hizo, El-Selhedar alizimia ghafla na mara moja akakimbizwa hospitalini. Baadaye alifariki katika hospitali ya Al-Amriya huko Alexandria na ikabainika mshtuko wa moyo ndio sababu ya kifo chake.

Wakati wa uhai wake, El-Selhedar alitumia muda mwingi wa taaluma yake na Ismaily katika miaka ya 1990 na kufanikiwa kutwaa mataji ya Ligi Kuu na mengine mengi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news