Rais Samia atajwa kuwa miongoni mwa wanawake 100 wenye nguvu kubwa Duniani

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

JARIDA la Forbes Africa limemtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa miongoni mwa wanawake 100 wenye nguvu Duniani.
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Awamu ya Sita wa Tanzania ambaye aliingia madarakani Machi,2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania toka mwaka 2015.

Rais Samia ameweka rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo wa juu zaidi nchini Tanzania.

Pia ni rais wa pili wa Tanzania kutokea Zanzibar, wa kwanza akiwa Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyeliiongoza Tanzania kwa miaka 10 kutoka mwaka 1985 mpaka 1995.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news