Ninaposema sijaja kutengua torati nina maana ya kuwa nimekuja kuongeza nguvu kiutendaji ili kumsaidia Mheshimiwa Rais kuboresha Utumishi wa Umma-Waziri Mhagama

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema amedhamiria kuimarisha misingi ya utendaji kazi kwenye Utumishi wa Umma ili wananchi wanufaike na huduma zitolewazo na taasisi za umma nchini.

Mhe. Jenista amesisitiza kuwa, ujio wake katika ofisi hiyo, sio wa kutengua torati, bali ni kuendeleza mazuri yaliyofanywa na mtangulizi wake na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha Utumishi wa Umma.

“Ninaposema sijaja kutengua torati nina maana ya kuwa nimekuja kuongeza nguvu kiutendaji ili kumsaidia Mhe. Rais kuboresha Utumishi wa Umma na kuendeleza mazuri yaliyokwishafanyika na watangulizi wangu,” Mhe. Jenista amesisitiza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news