Warembo wa SC wawakosesha raha wale wa Yanga SC, wakubali 4-1

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

WAREMBO wa Klabu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi, Simba Queens wamewachakaza watani wao, Yanga Princess.
Ni baada ya ushindi wa mabao 4-1 Januari 8,2022 katika mtanange wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Lite 2021/2022 ndani ya dimba la  Benjamin Mkapa katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam.
Aisha Djafar dakika ya saba na 82 na Opa Clement dakika ya 54 na 72 ndiyo waliopeleka maumivu kwa Yanga Princess.
Huku bao pekee la Yanga Princess likifungwa na Aisha Masaka kwa penalti dakika ya 76.

Chini ni msimamo wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Lite 2021/2022.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news