NA GODFREY NNKO
RAIS mstaafu wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt.Jakaya Kikwete amesema kuwa, kauli mbiu ya mwaka huu katika Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Uwekezaji Katika Sekta ya Madini inadhirisha nia ya Serikali ya kuifanya Sekta ya Madini iweze kutoa mchango unaostahili kwa Taifa.
Dkt. Kikwete ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla maalum ya Usiku wa Madini uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam amesema kuwa, kauli mbiu hiyo inaonesha dhamira ya kuiwezesha Sekta ya Madini itoe mchango stahiki kwa maendeleo ya Taifa letu tofauti na miaka ya nyuma.
"Pia inahakisi azma ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mama yetu mpendwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kusimamia mabadiliko ya kisera, mabadiliko ya kiutawala ili kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha kuvutia uwekezaji katika Sekta ya Madini barani Afrika.
Waziri Biteko
Awali, Waziri wa Madini Dkt.Doto Biteko amesema kuwa, Usiku wa Madini waliamua kuufanya kwa ajili ya kuwatambua wachimbaji madini wote nchini.
"Wachimbaji hawa kwa mwaka mzima, jambo wanalohubiriwa ni kuzingatia sheria, hili umekosea kuna faini, hili umekosea kuna hiki.Hawapati hata muda kidogo wa kuambiwa jambo jema, kwamba hongera umefanya vizuri,
Amesema kuwa, mafanikio yanayohubiriwa katika sekta ya madini yanatokana na juhudi za watu mbalimbali kwa kuweka msingi wa kuisimamia sekta hiyo ili iwe na manufaa makubwa kwa Taifa, hivyo wataendelea kuwathamini na kuwaheshimu viongozi wote waliotangulia katika kuisimamia wizara hiyo.
Pia amesema kuwa, mafanikio ya Sekta ya Madini yanatokana na maelekezo ya mara kwa mara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.
"Kama kuna mahali fulani yanachimbwa madini, basi mkulima wa maeneo yale apate masoko ya kuuza bidhaa zake, ule utaratibu wa kuchukua bidhaa zote kutoka nje ya nchi na kuzileta wakati Watanzania wana uwezo wa kuzizalisha, Mheshimiwa Rais anakemea tabia hiyo kwa nguvu zake zote, anataka Watanzania wanufaike na uwepo wa madini hayo.Mheshimiwa Rais metuelekeza vile vile kwenye ajira zozote zinazozalishwa katika nchi hii,sekta ya madini nayo ichangie,