Rais Samia atoa wito kwa Mahakama

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameitaka Mahakama kuzingatia sheria ili kutenda haki kwa watu wote bila kujali hali ya mtu kijamii na kiuchumi.
Rais Samia ameyasema hayo leo Februari 2, 2022 wakati wa kilele cha Maadhimisho Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Amesema, anatambua mageuzi yanayoendelea katika mahakama yameongeza uwazi na uwajibikaji kwa watendaji wa mhimili huo lakini bado yapo malalamiko kwa wananchi ya kucheleweshewa haki na wakati mwingine kunyimwa kabisa.
Mheshimiwa Rais amesema, malalamiko hayo yako hususani kwenye mirathi na hasa kutoka kwa wanawake wajane na migogoro ya ardhi.

Pia Rais Samia ameitaka mahakama kutoa haki bila kufungwa na masharti ya kiufundi ambayo wananchi wengi hawafahamu na wanategemea mawakili ndio wawaongoze.
Pia ameitaka Mahakama kutekeleza majukumu yake kwa kuangalia utu wa mtu kwa yule anayetoa hukumu na anayepewa.
“Utu wako unakutumaje uchukue fedha uminye haki ya mtu? Au umpe aliyetumia umahiri na vifungu kumyima haki mwenye haki,”amehoji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news