RC Hapi: Sitakubali mtu akwamishe maendeleo ya wananchi

NA FRESHA KINASA

MKUU wa Mkoa wa Mara,Ally Hapi amesema kuwa, kwa sasa hana mchezo na watendaji ama watumishi ambao wanakwamisha juhudi za Serikali za kuwaletea maendeleo wananchi.
Hapi amesema kuwa, hataogopa kumchukulia hatua kiongozi mzembe, fisadi, ama mla rushwa ambaye atabainika kufanya mambo ya ovyo na yasiyo na tija kwa maendeleo ya wananchi.
Ameyasema hayo leo Machi 2, 2022 wakati akizungumza katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji Mjini Musoma mkoani Mara, ambapo pamoja na mambo mengine amesema Serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa za kuwaletea maendeleo wananchi ikiwemo kutoa fedha za miradi ya maendeleo lazima ziwanufaishe wananchi.

"Kama kuna mtumishi anakula na mtu fulani nitamshughulikia kikamilifu na hakuna simu itakayopigwa. Rais anataka mkoa ubadilike, upige hatua kimaendeleo, mambo ya wizi au rushwa yaachwe. Mimi mwenzenu saizi nina raha kweli kweli nimekabidhiwa rungu na Mheshimiwa Rais sitaogopa kumchukulia hatua kiongozi yeyote bila kumuonea. Lazima tuweke msingi mzuri katika kuwatumikia wananchi wetu,"amesema Mheshimiwa Hapi.
"Kama viongozi wenzangu ndani ya Mkoa wa Mara hatutabadilisha mkoa huu kwa sasa hatutaweza kubadilisha wakati mwingine. Kama kuna tatizo tunalitatua na tunasonga mbele kwa pamoja, itafika wakati tuanze kushughulika na watu wanaochafua mkoa wetu, vijana acheni kutumika. Vyombo vya dola ingizeni makachero kwenye makundi hayo yanayofarakanisha watu bila ukweli wowote kusudi wanaofanya hivyo wachukuliwe hatua kali. Lazima tujenge msingi wa uadilifu haiwezekani kijana kuchafua mkoa kwa masilahi yake badala ya kufanya kazi za maendeleo,"amesema Hapi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news