TANZIA:Mwanafunzi Chuo Kikuu Iringa afariki

NA DIRAMAKINI

UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Iringa,umesema umepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha mwanafunzi wake, Hashim Komgisa Mzalilehi kupitia Idara ya Elimu Kitivo cha Sayansi na Elimu.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Afisa Habari na Masoko katika Chuo Kikuu cha Iringa (UoI).

"Uongozi unautaarifu Umma wa chuo kuwa msiba umetokea Jumamosi tarehe 23,4,2022 huko Mwanza, na mazishi (maziko) yatafanyika leo Jumapili 24,4,2022 Mwanza Sengerema.

"Uongozi wa chuo, unawapa pole wafiwa wote, na Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi,"imeeleza taarifa hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news