Afisa Maendeleo ya Jamii aliyepongezwa na Waziri Bashungwa apewa tuzo na Milioni 3/-

NA DIRAMAKINI

HALMASHAURI ya Manispaa ya Tabora mkoani Tabora imeungana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI),Mhe. Innocent Bashungwa kumpongeza Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Tabora Bi. Tumaini Mgaya kwa uongozi wake mahiri wa kuisimamia Idara ya Maendeleo ya Jamii.
Manispaa ya Tabora wamefanya hivyo ikiwa ni siki chache baada ya Mhe. Innocent Bashungwa kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Tabora kumuandalia Tuzo Maalum ya kutambua mchango wake katika idara hiyo akisema amekua Afisa Maendeleo bora na wa mfano.
Bi. Mgaya amekabidhiwa tuzo hiyo pamoja na shilingi milioni tatu. Awali, Waziri Bashungwa alieleza kuwa, kufanya hivyo kutatoa motisha kwa wengine kufanya kazi kwa bidii, umoja na mshikamano lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news