NA DIRAMAKINI
REFA Ahmed Arajiga wa Manyara ndiye atakayechezesha mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baina ya watani wa jadi, Simba na Yanga Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.


Kingilio cha
chini katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baina ya
watani, Simba na Yanga ni Sh. 10,000 Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza.
Taarifa ya TFF imesema viingilio vingine ni Sh, 30,000 VIP A na Sh, 20,000 VIP B na mchezo utaanza Saa 9:30 Alasiri.
0 Comments