BREAKING NEWS:Mahakama yawaachia huru watumishi watano TMDA

NA MWANANCHI

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewafutia kesi ya Uhujumu Uchumi na kuwaachia huru wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba nchini Tanzania (TMDA) akiwemo Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula, Raymond Wigenge, waliokuwa wanakabiliwa na shtaka moja la kuisababishia hasara mamlaka hiyo ya Shilingi milioni 58.
Hiyo ni baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza mahakama kuwa hana nia ya kuendelea na kesi dhidi ya washtakiwa hao.

Uamuzi wa kuifuta kesi hiyo umetolewa leo Mei 17, 2022 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Ritha Tarimo, wakati shauri hilo lilipoitwa mahakamani hapo kwa ajili ya kuendelea na ushahidi wa upande wa mashtaka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news