Je? Kuna huduma za matibabu kwa waathirika wa dawa za kulevya Tanzania

NA DIRAMAKINI

NDIYO, kwa mujibu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) kuna aina mbalimbali za matibabu kwa waraibu wa dawa za kulevya ingawa hakuna tiba moja ambayo inafaa kwa waraibu wote.

DCEA inaeleza kuwa, matibabu ya uraibu wa dawa za kulevya hutofautiana sana kulingana na aina ya dawa husika, kiasi cha dawa kilichotumika, muda wa uraibu, matatizo ya kiafya na mahitaji ya kijamii na mtu binafsi.

Huduma za tiba ya uraibu zinazotolewa nchini ni;

>Tiba saidizi kwa waraibu kwa kutumia dawa (Medically Assisted Therapy - MAT)
>Huduma katika Nyumba za Upataji Nafuu (Sober Houses)
>Tiba kwenye vituo vya kutolea Huduma za Afya ya Akili.

Hata hivyo, kwa mujibu wa DCEA kuna baadhi ya waraibu wanaopatiwa huduma za unasihi pekee kwenye asasi za kiraia na kuachana na matumizi ya dawa hizo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news