Katibu Mkuu Dkt.Jingu:Uwepo wa Safari Chaneli ni fursa ya kipekee kuitangaza nchi yetu

NA MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. John Jingu ameeleza kuwa uwepo wa Safari Chaneli ni fursa ya kipekee kuendelea kuitangaza nchi yetu ndani na nje na kuchagiza ukuaji wa uchumi.
Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara wadau wa Tanzania Safari Channel (TSC) kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Mei 30, 2022 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Dkt. John Jingu akiongoza kikao kazi cha Makatibu Wakuu wa Wiazra wadau wa Tanzania Safari Channel (TSC) walipokutana katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 30 Mei, 2022.

“Safari chaneli ni moja ya nyenzo ya kukuza utalii wetu na sisi kama wadau tuna jukumu la kuhakikisha tunawekeza vya kutosha katika maeneo muhimu ikiwemo rasilimali fedha zitakazosaidia kuendesha chaneli hii ili malengo ya uwepo wake yatimie,”alisisitiza Dkt. Jingu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi alieleza kuwa uwepo wa chaneli hiyo utasaidia katika kuvutia na kuongeza hamasa kwa watalii kuingia nchini.

“Tanzania Safari Channel ni msaada katika kuutangaza utalii, na kuitangaza nchi yetu na hii ni fursa kwetu nitoe wito kwa taasisi mbalimbali kuendelea kutangaza na kuitumia fursa hii ili kuendelea kukuza uchumi wetu,”alieleza Dkt. Yonazi
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi akichangia jambo wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara wadau wa Tanzania Safari Channel (TSC) Jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Lawrence Mafuru akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Kaspar Mmuya akifafanua jambo wakati wa kikao hicho.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Fatma Hamad Rajab alipongeza hatua ya uwepo wa chaneli ya hii, huku akieleza jitihada za Zanzibar kuanzisha chaneli ya utalii itakayosaidia kuitangaza na kuonesha vivutio vilivyopo.

“Kwa upande wa Zanzibar tuna mpango wa kuwa na chaneli ya ZBC 3 inayolenga kuonesha masuala ya utalii hatua hii inadhihirisha namna viongozi wetu kwa pande zote mbili wanavyojitahidi kutangaza vivutio vyetu vya utalii tunaahidi kuendelea kuwaunga mkono kwa kuhakikisha tunakuwa wabunifu katika kutangaza utalii wetu,”alisema Fatma.
Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayubu Ryoba akizungumza wakati wa kikao kazi cha Makatibu Wakuu wa Wizara wadau wa Tanzania Safari Channel (TSC) Jijini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara wadau wa Tanzania Safari Channel (TSC) wakifuatilia kikao hicho.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU).

Alihitimisha kuwa chaneli hizi zitasaidia kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu tamaduni zetu hivyo kudumisha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news