Madereva wanaohamasisha migomo wakalia kuti kavu, Chama cha Wasafirishaji (TAT) wasema kitakachowakuta shauri yao

NA DIRAMAKINI

CHAMA cha Wasafirishaji Tanzania (TAT) wiki hii kiliandaa mkutano wa vyama vyote vya wasafirishaji kulaani vitisho vya baadhi ya madereva wao wanaotangaza kugoma kazi na kuiomba Serikali ichukue hatua za haraka, kwani kauli za madereva hao zinachochea vurugu na kudhoofisha jitihada za ujenzi wa uchumi.
Katika siku za karibuni baadhi ya madereva wakiwa safarini ndani na nje ya Tanzania, wamekuwa wakirusha mitandaoni sauti zao wakisema wanagoma kazi wakidai, pamoja na mambo mengine, kulipwa mishahara, posho za safari na kuongezewa mafuta, mambo ambayo Rais wa TAT, Mohammed Abdullah, amesema mengine ni ya kimkataba.

Aidha,yanazungumzika na hayahalalishi vitisho vya kutelekeza magari na mizigo, mali ambazo wamekabidhiwa na wameaminiwa wazitunze. Kwa kina tazama sehemu ya kwanza hadi ya mwisho ya video ya taarifa hii ambayo imeandaliwa kwa msaada wa TAT TV (ambayo karibuni itakuwa hewani);

TAZAMA VIDEO:SEHEMU YA 1-4 TAT

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news