TARURA YATEKELEZA AGIZO LA BASHUNGWA LA KUJENGA DARAJA LILILOKUWA LIKIHATARISHA MAISHA YA WANAFUNZI

NA OR-TAMISEMI

WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) mkoani Njombe umekamilisha ujenzi wa daraja linalounganisha kata za Ramadhani na Njombe Mjini ambalo kilikuwa hatari kwa watumiaji kutokana na kutandikwa matapa.
Awali watumiaji wa daraja hilo wanasema madereva wa vyombo vya moto na wanafunzi walikuwa wakitumbukia mtoni wakati wa mvua kubwa ambazo zilikuwa zikifunga njia.

Kutokana na hali hiyo mwanzoni mwa mwaka huu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Innocent Bashungwa alifikuwa katika daraja hilo na kumtumbua aliyekuwa Meneja wa TARURA mkoani humo kisha kuhamishiwa Mkoa wa Ruvuma kwa kuchelewa kutekeleza mradi huo uliokua umeshapatiwa fedha kipindi alipokuwa mkoani Njombe kabla ya kuhama.

Hivi sasa wananchi wanafurahia ujenzi huo ambapo wanasema imerahisisha usafiri kwa wao kuweza kusafirisha biashara zao na kuongeza usalama kwa wote wanaotumia barabara hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news