Yanga SC kumenyana na Simba SC nusu Fainali Kombe la TFF Mei 28

NA MWANDISHI WETU

NUSU Fainali za Kombe la Shirikisho Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup zitafanyika mwishoni mwa mwezi huu Arusha na Mwanza.
Nusu Fainali ya kwanza baina ya watani wa jadi, Simba ambao ni mabingwa watetezi na Yanga itachezwa Mei 28 Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wakati ya pili itafuatia Mei 29 baina ya Azam FC na Coastal Union Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mwaka jana Simba waliifunga Yanga katika fainali 1-0 Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, bao pekee la kiungo Mganda, Thadeo Lwanga.
Aidha, fainali ya mwaka huu itafanyika Julai 2, mwaka huu katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news