Bao la Pape Ousmane Sakho wa Simba SC latua CAF

NA DIRAMAKINI 

WINGA raia wa Senegal anayekipiga katika Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Pape Ousmane Sakho kupitia bao alilofunga dhidi ya ASEC kwenye mechi ya Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika limeingia kwenye kipengele cha kuwania Bao Bora la Mwaka Afrika katika Tuzo za Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Pape Ousmane Sakho alifunga bao hilo dakika ya 12 tu akimalizia krosi ya beki wa kulia, Shomari Kapombe katika ushindi wa 3-1 dhidi ASEC Mimosas ya Februari 13, mwaka huu Uwanja wa Benjamin Mkapa uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news