Watanzania waziona fursa, Mhe.Makinda azindua saluni ya kisasa mjini Shinyanga

NA KADAMA MALUNDE

SPIKA wa Bunge mstaafu Mhe. Anne Makinda amezindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga huku akimpongeza mmiliki wa Saluni hiyo Adam Mwihechi kwa uwekezaji huo ambao umewezesha kupatikana kwa ajira 25 za vijana.
Muonekano wa sehemu ya kunyolea nywele ndani ya Big 5 Barbershop & Sauna.

Makinda ambaye ni Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 ametoa pongezi hizo leo Jumamosi Julai 2,2022 akielekea kwenye Bonanza la Sensa ya Watu na Makazi 2022 lililoandaliwa na kundi la mtandao wa Kijamii maarufu SHY TOWN VIP Mjini Shinyanga.

“Nakupongeza kwa ubunifu huu, hii ni sehemu nzuri na haujasema siri uliyaona wapi haya mambo mazuri ukaamua kuyaleta hapa, ni saluni ya kisasa ambayo kila mtu lazima afurahie huduma, nimeona wafanyakazi wana furaha. Wengi wetu tutakuja kupata huduma hapa kwani kuna huduma nzuri na panafurahisha sana”.
Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akiwa amekaa kwenye kiti ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga.

“Nakushukuru kwa kuajiri vijana 25 kwani umeleta ajira kwa vijana hawa. Naomba vijana mfanye kazi kwa bidii, kushirikiana na kujituma”,amesema Makinda.

Makinda ametumia fursa hiyo kumshauri mmiliki wa Saluni hiyo ya kisasa kutumia mitandao ya kijamii kutangaza huduma anazotoa huku akiishukuru Benki ya NMB kwa kumpatia mkopo mmiliki wa Saluni hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi na Mmiliki wa Big 5 Barbershop & Sauna bw. Adam Mwihechi amemshukuru Mhe. Anne Makinda kwa kuzindua saluni ya kisasa ‘iliyoboreshwa zaidi’ akisema sasa ina viwango vya kimataifa.
Mkurugenzi wa Big 5 Barbershop & Sauna, Adam Mwihechi (kushoto) akimuonesha Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda vifaa mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga 
Mkurugenzi wa Big 5 Barbershop & Sauna, Adam Mwihechi (kushoto) akimuonesha Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda vifaa mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga 

Amezitaja huduma wanazotoa kuwa ni huduma zote za saluni ambapo sasa wana sehemu maalumu ya kuhudumia watoto, na chumba maalumu kwa kuhudumia mtu mmoja “VIP” na huduma zingine kede kede ikiwemo Barbershop, kuosha miguu, Gym, Game Centre, Sauna, Massage na muziki.

“Tunawashukuru sana Benki ya NMB wameendelea kutushika mkono kwa kutupatia mkopo na sasa tunaendelea kupanua huduma na kuzifanya kuwa za kisasa zaidi,”amesema Mwihechi.
Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akikata utepe kuzindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, kulia ni Mwenyekiti wa SHY TOWN VIP, Mussa Ngangala. 
Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akizindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022. Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, kulia ni Mwenyekiti wa SHY TOWN VIP, Mussa Ngangala. 
Mwenyekiti wa SHY TOWN VIP, Mussa Ngangala akizungumza wakati Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda (kulia) akizindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022. 
Mkurugenzi wa Big 5 Barbershop & Sauna, Adam Mwihechi (kushoto) akizungumza wakati Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akizindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022. 
Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akiwa ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna iliyoboreshwa zaidi Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022 baada ya kuizindua.
Wafanyakazi wa Big 5 Barbershop & Sauna wakifuatilia matukio wakati Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akizindua Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga leo Julai 2,2022. 

Naye Afisa Mahusiano wa Benki ya NMB tawi la Manonga, William Tumbo amesema benki hiyo imekuwa ikitoa ushirikiano kwa Big 5 Barbershop & Sauna kwa kuipatia mikopo yenye riba nafuu tangu mwaka 2013 huku akiwasihi wananchi kuchangamkia fursa zinazotolewa na benki hiyo.
Mkurugenzi wa Big 5 Barbershop & Sauna, Adam Mwihechi (kushoto) akimuonesha Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda vifaa mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga. 
Mkurugenzi wa Big 5 Barbershop & Sauna, Adam Mwihechi (kushoto) akimuonesha Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda vifaa mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga 
Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Anne Makinda akiwa ndani ya Saluni ya Kisasa maarufu Big 5 Barbershop & Sauna Mjini Shinyanga. 
Afisa Mahusiano wa Benki ya NMB tawi la Manonga, William Tumbo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Big 5 Barbershop & Sauna.

Big 5Barbershop & Sauna ipo pembezoni mwa barabara ya Mwanza – Shinyanga jirani na Jengo la NSSF Mjini Shinyanga. Wasiliana nao kwa simu namba 0767446337.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news