Mtume Mwamposa:Sensa ni jambo la baraka kiimani, wakati Yesu anazaliwa ilitangazwa amri na Kaisari kuwa watu wote wahesabiwe

NA DIRAMAKINI

KIONGOZI wa Kanisa la Inuka Uangaze (Arise and Shine),Nabii na mtume Boniface Mwamposa (Bulldozer) ameweka bayana utayari wake katika zoezi la kuhesabiwa kupitia Sensa ya Watu na Makazi Agosti 23, mwaka huu.
Mwamposa ambaye amekuwa kiongozi mahiri wa imani ya Kikristo nchini hata kujizolea umaarufu mkubwa kama "Bulldozer" ameeleza namna zoezi la sensa lilikuwa likifanyika hata zamani katika vitabu vitakatifu vinajieleza na kuwaasa watanzania kutopotoshwa juu ya zoezi la kuhesabiwa nchini.

"Sensa ni jambo la baraka kiimani, wakati Yesu anazaliwa ilitangazwa amri na Kaisari kuwa watu wote wahesabiwe, hata Yesu alipozaliwa alizaliwa katika holi la ng'ombe sababu nyumba za wageni zilijaa watu waliokuwa wamerudi kwao kuhesabiwa,"amesema.

Mchungaji Mwamposa amewaasa watanzania kujitokeza kuhesabiwa na kufurahia jambo hilo kwani linaleta baraka kwa wananchi na nchi kiujumla.

"Furahia kuhesabiwa ili ujulikane kama mmoja wa watanzania walio mchini, mimi,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news