Prof.Muhongo ahesabiwa na wanakaya yake Musoma Vijijini

NA FRESHA KINASA

MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini mkoani Mara, Prof. Sospeter Muhongo na wanakaya yake walioamkia nyumbani leo Agosti 23,2022, tayari wahesabiwa.

Mheshimiwa Prof. Muhongo amesema waliohesabiwa ni wanakaya sita na wageni wawili. "Karani anafanya kazi yake kwa weledi mkubwa sana. Wanakaya na wageni wote wamejibu maswali yote kwa usahihi unaotakiwa.

"Watanzania wote tuendelee kuhesabiwa kwa faida yetu na maendeleo ya nchi yetu.Ukweli na takwimu za kuaminika na zisizo na shaka ni hitaji la lazima kwa mipango, bajeti, miradi na programu zozote zinazohitajika, zenye maandalalizi mazuri na misingi imara,"amesema Prof.Muhongo.

Picha za hapa chini zinawaonesha watu nane waliohesabiwa nyumbani kwa Prof.Muhongo. Karani nae yuko pichani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news