Rais Dkt.Mwinyi aongoza maziko ya Mke wa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na wananchi katika kupokea jeneza likiwa na mwili wa marehemu Hamida Mussa Omar. Mke wa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Faina Idarous (kushoto kwa Rais) na kulia kwa Rais ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, kwa ajili ya kusalia, sala hiyo iimefanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Donge Karange Mkoa wa Kaskazini Unguja leo Agosti 7, 2022.(Picha na Ikulu).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na waumini wa Dini ya Kiislam katika ibada ya sala ya jeneza ikiongozwa na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Donge Karange Mkoa wa Kaskazini Unguja leo, kushoto kwa Rais ni mume wa mareheme Hamida Mussa Omar, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Faina Idarous, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na kulia kwa Rais ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Sheikh.Hassan Othman Ngwali na Makamu wa Kwanza wa Rais, Mhe. Othman Masoud Othman.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na waumini wa Dini ya Kiislam wakiitikia dua ikisomwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Sheikh.Hassan Othman Ngwali (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya jeneza , iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Donge Karange Mkoa wa Kaskazini Unguja leo,kushoto kwa Rais ni mume wa marehemu Hamida Mussa Omar, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,. Faina Idarous, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla. (Picha na Ikulu).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la marehemu Hamida Mussa Omar, wakati wa maziko yaliofanyika Kijiji cha Donge Karange Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.(Picha na Ikulu).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akishiriki katika kuitikia dua ya kumuombea marehemu Hamida Mussa Omar, baada ya kumalizika kwa maziko yaliyofanyika katika Kijiji cha Donge Karange Mkoa wa Kaskazini Unguja leo, kulia kwa Rais ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Othman Masoud Othman na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mhe, Ayoub Mohammed Mahmoud na kushoto kwa Rais ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Hemed Suleiman Abdulla.(Picha na Ikulu).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akitoa mkono wa pole kwa familia ya marehemu Hamida Mussa Omar, Mke wa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Faina Idarous (kulia kwa Rais) alipofika nyumbani kwa marehemu Donge Karange na kushoto kwa Rais ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news