Siku tatu za CCM Dodoma

NA DIRAMAKINI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kuwataarifu wanachama wake na watanzania wote kuhusu kufanyika kwa vikao vya kawaida vya uongozi ngazi ya Taifa Jijini Dodoma kuanzia tarehe 26 Septemba, 2022 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (CC) na tarehe 27 na 28 Septemba, 2022 Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa (NEC).

Pamoja na mambo mengine vikao hivi vitakuwa na kazi ya kupokea mapendekezo, kujadili, kupitisha na kufanya uteuzi wa mwisho wa wanachama ambao wameomba uongozi katika ngazi ya wilaya.

Vikao hivyo vilitanguliwa na kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Kilichofanyika tarehe 22 na 23 Septemba, 2022 Jijini Dodoma.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Shaka Hamdu Shaka
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA, ITIKADI NA UENEZI.
25 Septemba, 2022.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news