WAWEKEZAJI ARUSHA WAMWAGIA SIFA RAIS SAMIA UJENZI WA BARABARA ZA TARURA

NA MWANDISHI WETU

WAWEKEZAJI na wananchi wa Kata ya Themi, Halmashauri ya Jiji la Arusha wamemsifu na wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali na kuwajengea kwa kiwango cha lami barabara za Themi -Viwandani zenye urefu wa kilometa 1.4 kwagharama ya shiligi 1,175,141,850.00.
Pongezi hizo zimetolewa wakati wa ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja jijini Arusha iliyofaywa na bodi ya ushauri ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA).

Akitoa pongezi hizo mkurugenzi wa “Spanish Tiles” Bobby Chadha alisema kuwa anamshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali na kuwapatia barabara nzuri na bora za lami maeneo ya viwandani.
"Ninamshukuru sana rais kwa sababu kwa mara ya kwanza tumepata barabara hizi za lami kwa zaidi ya miaka 40 niliyokuwa hapa. Barabara hizi zitasaidia sana kupungza gharama za usafiri, kukuza biashara na pia kupendezesha mji,” alisema Bobby.

Naye ndugu Satbir Hanspaul mkurugezi mtendaji wa “Hanspaul Group” alisema kuwa anamshukuru na kumpongeza sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu walikuwa wanapata changamoto kubwa sana kwa magari kufika viwandani na magari mengi yalikuwa yanaharibika lakini sasa barabara imewaondolea kero hizo.
"Wageni walikuwa wakija eneo la Kiwanda na kuona miundombinu mibovu walikuwa wanapata wasiwasi na kiwanda pia, lakini tumeona Serikali yetu imeona changamoto na kuifanyia kazi haraka, sasa tunaaminika kwa sababu mazigira yameboreshwa,” alisema Hanspaul.

Mama Veronica Saimon mfanyabiashara wa eneo la viwandani alisema kuwa kabala ya barabara haijajengwa walikuwa wakipata shida sana kutokana na vumbi jingi pamoja na matope wakati wa mvua hali iliyokuwa inaathiri biashara yao.
Alieleza kuwa kwa sasa anamshukuru sana Rais Samia kwa kuwajali, sababu kwa sasa wanafanyabishara bila shida na wateja wengi wanawapata baada ya barabara kujengwa.

Kwa upande wake Mhe. Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini aliwashukuru watendaji na wataalamu wa TARURA kwa kazi kubwa wanayofanya na ameona tofauti kubwa sana baada ya TARURA kuanzishwa.
"Huko nyuma kaba ya kuanzishwa TARURA ilikuwa ngumu kupeleka mradi sehemu inayoeleweka na ukaleta tija kwa sababu kila diwani alikuwa akivutia upandewa wake. Leo mmewasikia hapa wawekezaji wamesubiri barabara kwa takribani miaka 40 lakini baada ya TARURA kuanzishwa barabara imejengwa,"alisema Mhe. Gambo.

Aidha alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa Kuendelea kuenzi falsafa ya Serikali ya “Tanzania ya Viwanda” kwa kuboresha miundombinu katika maeneo hayo ya viwandani yenye viwanda zaidi ya 20, ambapo ajira zinaogezeka na uchumi wa wanachi wa maeneo ya viwandani wanaofikia takribani 11,000 unaboreka.
Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff kwa upande wake alisema kuwa wamejipanga kuwafikia wannachi katika sehemu ambazo hazifikiki na pia katika maeneo ya kimkakati.

“TARURA tunakufikisha kusikofika lakini nasema pia Penye nia pana njia na pasipo na njia TARURA tupo,"alisema Mhandisi Seff.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news