377 wakamatwa kwa kujihusisha na dawa za kulevya, mali zataifishwa

NA DIRAMAKINI

JESHI la Polisi Tanzania kupitia Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (Anti Drugs Unit) kwa kushirikiana na polisi mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wa dawa za kulevya pamoja na vifaa mbalimbali.
Mkuu wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Kamishina Msaidizi wa Polisi, ACP AMON KAKWALE amesema kuwa,kuanzia mwezi Julai hadi Novemba, 2022, jumla ya kesi 369 zilifikishwa mahakamani na kutolewa uamuzi.
Amebainisha kuwa, jumla ya watuhumiwa 377 walitiwa hatiani kwa makosa ya kujihusisha na dawa za kulevya.Pia amesema watuhumiwa 170 walifungwa vifungo mbalimbali kwa makosa hayo.

ACP Kakwale ameongeza kuwa, vyombo vya moto vilivyokamatwa na kutaifishwa ni magari nane, pikipiki tisa, boti mbili na nyumba moja vilitaifishwa na Mahakama kuwa mali za Serikali.
Pia amesema, jeshi hilo halitomuonea huruma mtu yeyote atakayekamatwa akijihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya na jeshi hilo linawaomba wananchi kutoa taarifa za watu wachache wanaojihusisha na matukio ya uhalifu ili hatua zichukuliwe dhidi yao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news