
Amesema kundi la watu wenye ulemavu linapaswa kupewa kipaumbele kwa kuzingatia michango waliyonayo katika jamii huku akieleza namna Taasisi yake ilivyolifikia kundi hilo.
"Kwa kutambua michango ya watu wenye ulemavu tutaendelea kuwashirikisha ili wapewe nafasi ya kutoa michango yao katika jamii na maendeleo ya nchi,"alisisitiza.
Alifafanua kuwa, kundi hili ni sehemu muhimu katika jamii hivyo waendelee kuhusishwa katika mipango na mikakati mbalimbali kama inakifanyika kwa watu wengine.
Aidha, alitumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali kwa jitihada za kuhakikisha inaboresha mazingira ya watu wenye mahitaji maalumu kwa kuzingatia Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 inayotambua nafasi ya watu wenye ulemavu katika kuchangia maendeleo ya nchi na inawahamasisha kutumia fursa mbalimbali zinazojitokeza ili kujikwamua kiuchumi.
“Kipekee naipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwa jitihada wanazozifanya katika utekelezaji wa dhana ya afya Moja kuwa shirikishi, nitoe rai kwa wadau kuendelea kuunga mkono jitihada hizi,"alisisitiza.
Pamoja na hayo aliwaomba wadau kuendelea kushirikiana na Taasisi ya TAMIPA katika kuhudumia wenye mahitaji maalum.