Uingereza yatinga robo fainali kwa kuichapa Senegal 3-0

NA DIRAMAKINI

NAODHA wa Uingereza, Harry Kane amefunga bao lake la kwanza dakika ya tatu ya kipindi cha pili katika Kombe la Dunia la Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) 2022 nchini Qatar, akiisaidia timu yake kuishinda Senegal mabao 3-0.
Mashabiki wa Senegal wakiwa na huzuni baada ya matokeo hayo.(Picha na Sorin Furcoi/Al Jazeera).

Ushindi huo umepatikana Desemba 4, 2022 katika dimba la Al Bayt lililopo Doha, Qatar hivyo kutinga robo fainali ya michuano hiyo mikubwa duniani. Pia ushindi huo, ni hatua ya maandalizi kwa mechi dhidi ya Ufaransa katika robo fainali.

Kane alifunga kwa mara ya 52 kwa nchi yake kuingia ndani ya rekodi moja ya Wayne Rooney. Pia alimpita Gary Lineker kama mfungaji bora wa nchi yake katika mashindano makubwa akiwa na mabao 11.

Jordan Henderson ndiye alianza dakika ya 38 na Bukayo Saka akahitimisha tabasamu la Senegal dakika ya 57 katika dimba la Al Bayt huku Jude Bellingham akicheza nafasi muhimu kufanikisha ushindi huo.

Uingereza, ambayo ilitinga nusu fainali katika Kombe la Dunia lililopita nchini Urusi mwaka 2018, itamenyana na mabingwa watetezi Ufaransa kwenye Uwanja wa Al Bayt siku ya Jumamosi hii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news