Waziri Dkt.Kijaji ateta na Balozi Jatmiko wa Indonesia

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji baina ya Tanzania na Indonesia na Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Tri Yogo Jatmiko.
Mheshimiwa Dkt.Kijaji amefanya mazungomzo hayo na Balozi Jatmiko leo Desemba 6, 2022 katika Ofisi za wizara jijini Dodoma.
Waziri Kijaji amemhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania iko tayari kuendeleza ushirikiani baina ya nchi hizo na iko tayari kuwezesha miradi ya uwekezaji hususani katika sekta ya kilimo hasa katika uongezaji wa mnyororo wa thamani katika mazao ambayo nchi hiyo imepanga kuyaendeleza kama vile karafuu ili kuongeza ajira na kipato kwa wanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news