Mhandisi Dkt.Mngereza azungumzia Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Zanzibar 2022-2027

NA MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi (WAMM), Mhandisi Dkt.Mngereza Mzee Miraji amesema Mpango wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Zanzibar 2022-2027 wenye lengo la kuimarisha sekta ya maji na kumaliza tatizo la maji safi na salama Zanzibar alianzisha kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo mbalimbali.
Mhandisi Dkt. Mngereza aliyasema hayo jana katika hafla iliyoandaliwa ya kumkabidhiwa Tuzo ya Kifahari ya VIP Global Water Change Maker, Mhe Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi iliyofanyika Ikulu jijini Zanzibar.

Alisema katika kipindi ulichoteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini alichukuwa juhudi mbalimbali za kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama, kwa kukutana na Mashirika ya Kimataifa ya Misaada ikiwemo JICA, USAID, BPI, Banks ikiwemo AFDB, wawakilishi wa balozi mbalimbali ikiwemo UK, EU, JAPAN n.k.
Alielezea kwamba hivyo Wizara ya Maji, Nishati na Madini (WMNM) na Taasisi ya Ushirika wa Wadau wa Maji (GWP ) walishirikiana kuandaa mpango huo uliojumuisha wataalam wa fani mbalimbali kutoka Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Tanzania (SMT), South Afrika na Ethiopia chini ya ufadhili wa GWP ambapo mshauri elekezi wa kikosi alikuwa Dkt.Victor Kongo.
Aliesema kuzinduliwa kwa Mpango huo pamoja na kuutangaza kwa kufanya Makongamano na Warsha mbali mbali kulipelekea Washirika wa Maendeleo kujitokeza na kuonesha nia ya kuunga mkono Serikali Zanzibar katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama. 

Mhandishi Dkt Mngereza alisema Miongoni mwa Washirika wa Maendeleo walijitokeza ni pamoja na KFW na GIZ za Ujerumani, Ruden Institute ya Norway, UNESCO-IHI Delft ya Uholanzi, JICA ya Japani na Benki ya EXIM India.

Aidha alimshukuru Rais Mstaafu Jakaya Mrisho, kupitia GWP kwa juhudi zake za kubeba jambo hili kwa hatua zote,alipokuwa Dakar,nchini Senegal aliagiza utekelezaji wa hilo na baada ya muda mfupi alipatikana na kuanza kazi, May-Nov 2022.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ushirika wa Wadau wa Maji (GWP ) Dkt Victor Kongo alisema zoezi la Mpango Mkuu wa maji lilikua gumu kidogo kwani ilibidi watafute nyaraka na ripoti mbali mbali kuanzia miaka ya 60 iliyopita hadi sasa ili kutambua miundo, mifumo na mipangilio iliyopo ya usimamizi wa sekta ya maji Zanzibar na changamoto zake. Pia, walifanya tathmini kutambua wingi na ubora wa rasilimali maji Zanzibar na changamoto za usimamizi wake. 

Alisema kupitia mashirikiano mazuri na taasisi ya Global Water Partnership, Dkt. Mngereza aliweza kuhudhuria kikao cha dunia cha World Water Forum kule Dakar Senegal ambapo alikutana na wadau wa kimataifa katika sekta ya maji. 
Alifahamisha kwamba wadau hao ni pamoja na mkuu wa chuo cha kimataifa cha IHE-Delft kilichoko Uholanzi ambacho ni hodari katika utafiti na taaluma katika sekta ya maji. 

Alisema Pia kupitia chuo hicho pamoja na taasisi ya SADC Groundwater Monitoring Institute, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Wizara ya Maji nishati na Madini walianzisha kongamano la kila mwaka la kisayansi kuhusu maji Zanzibar ambalo lilifanyika kwa mara ya kwanza tarehe 14-15 Septemba mwaka 2022 na litakuwa likifanyika kila mwaka.
Alifahamisha tathmini waliyoifanya ilibainisha mambo makuu saba kati ya mambo hayo ikiwemo athari za mabadiliko ya tabia nchi katika sekta ya maji Zanzibar, Kwa muda mrefu, hakujakuwa na mpangilio maalum au Programme ambayo ina ratibu mwenendo wa utekelezaji wa miradi katika sekta ya maji. Hali ambayo ilisababisha kutokuwa na muelekeo maalum wenye malengo katika sekta ya maji. 

Vile vile alisema Sera ya maji ya 2004 ina mapungufu kadhaa ambayo inatakiwa kushughulikiwa kwa kufanya mapitio ya hiyo sera. Pia Kunahitajika hatua madhubuti za kuboresha miundo mbinu iliyopo na pia kuongeza miundo mbinu mipya ya kusambaza maji.

Sambamba na hayo hatua madhubuti zinahitajika kujenga mashirikiano na taasisi za kikanda na kimataifa katika sekta ya maji ili kupanua wigo wa mashirikiano ya kitaaluma na utafiti.
Aidha, Dkt.Mngereza na Dr Victor wamempongeza Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi kuwa Mpokeaji wa Kwanza wa Tuzo ya Kifahari ya VIP Global Water Change Maker, pamoja kuwa pongeza viongozi wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini kwa Kuendeleza utekelezaji wa Mpangu Mkuu wa Maji Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news