TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA NCHI ZA EAC KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI ZIWA VICTORIA

NA MWANDISHI WETU

JAMHURI ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha rasilimali za uvuvi katika Ziwa Victoria zinalindwa ili zinufaishe jamii zinazozunguka ziwa hilo na mataifa husika kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

Prof. Shemdoe aliuhakikishia mkutano huo kuwa, Tanzania itaendelea kuchukua hatua madhubuti za kusimamia ziwa hilo kama nchi wanachama wa wa LVFO zilivyokubaliana. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.

Alisisitiza pia kuwa Tanzania inaendelea kudhibiti matumizi ya zana haramu za uvuvi, kupiga marufuku uvuvi wa samaki wachanga, kudhibiti utoroshaji wa mazao ya uvuvi na kuhamasisha ufugaji wa samaki kwa vizimba katika Ziwa Victoria bila kuathiri mazingira. 

Amesema pia, Tanzania imeimarisha udhibiti wa uingizaji wa zana za kuvulia samaki ili kuzuia uingizaji wa zana haramu nchini na kuendesha ukaguzi wa kina ili kuhakikisha uvuvi endelevu unafanyika kwa tija.
Makatibu Wakuu ambao ni Wajumbe wa kamati ya Uratibu ya Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 19, Aprili jijini Kampala, Uganda.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu ukifuatilia Mkutano huo.

Pia Profesa Shemdoe alitanabaisha kuwa mchango wa Sekta za Uvuvi katika uchumi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mdogo sana kwakuwa mchango wake unahesabiwa katika maeneo ya uvuvi na ukuzaji bila kujumuisha mapato yanayotokana na shughuli zote zinazofanyika katika minyororo yake ya thamani.

“Mchango wa Sekta za Uvuvi katika uchumi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mdogo sana kwakuwa mchango wake unahesabiwa katika maeneo ya uvuvi na ukuzaji bila kujumuisha mapato yanayotokana na shughuli zote zinazofanyika katika minyororo yake ya thamaniBadala yake thamani hiyo inajumuishwa katika sekta zingine na hivyo kutokutoa picha halisi ya Sekta ya Uvuvi,” alisema.
Ujumbe wa Uganda (kushoto) na ujumbe wa Tanzania (kulia) katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu ukifuatilia Mkutano huo.
Washiriki wa Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu wakifuatilia Mkutano huo.

Katika mkutano huo, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uganda, Dkt. Aziz Mlima, alimwakilisha Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo.

Kikao hiki kimehudhuriwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zilizopo katika Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news