VIDEO:Rais mteule wa TLS,Wakili Harold Sungusia ataja mambo matano

NA DIRAMAKINI

WAKILI Harold Sungusia amechaguliwa kuwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) katika uchaguzi uliofanyika ljumaa Mei 12, 2023 kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka 2023 unaofanyika jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha wanasheria Tanganyika,Wakili Charles Rwechungura ndiye aliyemtangaza Harold Sungusia kuwa rais mpya wa chama hicho baada ya matokeo ya uchaguzi, huku nafasi ya Makamu wa rais ikichukuliwa na Aisha Sinda.

Aidha,kati ya kura zilizopigwa 825 hakuna iliyoharibika ambapo Harold Sungusia alipatata kura 748 huku Reginald Shirima akipata kura 77.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news