Waziri Ummy ataja faida za umeme wa uhakika kwa Sekta ya Afya

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu amepongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nishati Mhe. Januari Makamba na watendaji wote katika Sekta ya Nishati kwa kuendelea kuhakikisha watanzania wanapata nishati ya umeme ambayo pia inasaidia katika uboreshaji wa huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Waziri Ummy amesema hayo mara baada ya kutembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwenye maonesho ya Wiki ya Nishati inayoendelea kufanyika jijini Dodoma katika viwanja vya Bunge.
“Upatikanaji wa umeme wa uhakika unasaidia pia katika kuboresha huduma za matibabu katika vituo vya kutolea huduma za afya hivyo kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa uharaka zaidi kwa kutumia vifaatiba,”amesema Waziri Ummy.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news