Tanzania yaadhimisha Siku ya Yoga Duniani

NA ELEUTERI MANGI-WUSM

TANZANIA imeadhimisha Siku ya Yoga Duniani huku Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ikisisitiza kuunga mkono sherehe za kitamaduni za mataifa mbalimbali duniani kwa sababu zinasaidia kujenga jamii ya kimataifa kuwa wamoja.
Hayo yamsemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu wakati wa maadhimisho ya Siku ya Yoga Duniani ambayo huadhimishwa Juni 18, kila mwaka ambapo kwa Tanzania yamedhuiriwa na watu mbalimbali ambao wamefanya mazoezi ya Yoga kwa pamoja katika viwanja vya Gym Kana jijini Dar es Salaam.
“Huu ni mwaka wa tisa sasa tangu Umoja wa Mataifa ulipotambua na kuupa mchezo wa Yoga siku maalum, Ubalozi wa India umeandaa sherehe hizi ambazo zimehuidhuriwa na watu zaidi ya 1000 kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo India na Tanzania,”amesema Bw. Yakubu.
Mchezo wa Yoga asili yake ni India unaosaidia kuufanya mwili kuwa imara kwa kupata mazoezi kuanzia kichwani hadi miguuni hatua inayofanya mwili kuwa imara na kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza. 
Miongoni mwa washiriki wa maadhimisho hayo ni Balozi wa India nchini Bw. Binaya Srikanta Pradhan na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini nchini Bw. Zlatan Milišić ambapo kwa Tanzania Siku ya Yoga imeadhimishwa katika mikoa ya Tanga, Dar es salaam, Morogoro, Dodoma, Mwanza, Arusha, Zanzibar na Kilimanjaro.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news