Tanzania yafanya upasuaji wa moyo nchini Zambia

Madaktari bingwa wa usingizi na wagonjwa mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia wakimlaza mgonjwa kwaajili ya kufanyiwa upasuaji wa moyo. Upasuaji huo umefanyika hivi karibuni nchini Zambia ambapo wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya Moyo Zambia walifanya upasuaji wa kuondoa uvimbe kwenye chumba cha juu upande wa kushoto wa moyo (Myxoma). Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child's Heart -SACH) la nchini Israel ndilo lililoratibu ufanyikaji wa upasuaji huo. 
Wataalamu wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuondoa uvimbe kwenye chumba cha juu upande wa kushoto wa moyo (Myxoma).Upasuaji huo umefanyika hivi karibuni nchini Zambia ambapo wataalamu wa JKCI walifanya upasuaji kwa kushirikiana na wenzao wa hospitali ya Taifa ya Moyo ya Zambia. Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child's Heart -SACH) la nchini Israel ndilo lililoratibu ufanyikaji wa upasuaji huo. 
Daktari bingwa wa wagonjwa wa dharura na mahututi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Vivian Mlawi akiwafundisha wataalamu wa afya wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura na mahututi wakati wataalamu wa JKCI walipokwenda katika Hospitali hiyo kwaajili ya kufanya upasuaji wa moyo na kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya. Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child's Heart -SACH) la nchini Israel ndilo lililoratibu ufanyikaji wa upasuaji huo. 

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia, Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child's Heart -SACH) la nchini Israel na Congenital Heart Academy kutoka nchini Italia wakiwa katika kikao cha kuangalia ni namna gani JKCI itakavyowajengea uwezo wataalamu wa hospitali hiyo ili waweze kutoa huduma za upasuaji wa moyo.
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Taifa ya Moyo ya nchini Zambia, Shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child's Heart -SACH) la nchini Israel na Congenital Heart Academy kutoka nchini Italia wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kuangalia ni namna gani JKCI itakavyowajengea uwezo wataalamu wa hospitali hiyo ili waweze kutoa huduma za upasuaji wa moyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news