Dkt.Jingu ateta na wawakilishi wa NIRAS Tanzania, Umoja wa Ulaya

NA MWANDISHI WMJJWM

KATIBU Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt.John Jingu amekutana na kufanya Mazungumzo na Mwakilishi wa shirika la linalojishughulisha na masuala ya jinsia la NIRAS Tanzania, Dkt. Suma Kaare pamoja na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya, Guidet Chiara leo Julai 3, 2023 jijini Dodoma.
Kikao hicho kilikua na lengo la kuwatambulisha wataalam wasaidizi sita wa shirika hilo watakaofanya kazi kwa kushirikiana na Serikali kutekeleza Mradi wa GENDER TRANSFORMATIVE ACTION, BREAKING THE GLASS CEILING IN TANZANIA, unaofadhiliwa na umoja wa Ulaya ili kutekeleza afua za kupinga ukatili na kuwezesha usawa Kijinsia nchini.
Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Wakili Amon Mpanju na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Sifuni Msangi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news