Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade amuongoza RC Balozi Dkt.Buriani katika mabanda mbalimbali

NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Tabora, Mhe.Balozi Dkt.Batilda Buriani ametembelea Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) ambapo alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Bi.Latifa Khamis ambaye alimuongoza katika kutembelea mabanda mbalimbali ikiwa ni pamoja na Banda la Bidhaa za Asali. 
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Balozi Dkt. Batilda amepongeza bidhaa zilizooneshwa katika banda la asali na kusema kuwa ni za viwango vya juu na nyingi zinazalishwa katika Mkoa wa Tabora. 
Pia akiwa katika Banda la Shirika Umeme Tanzania (TANESCO), Mhe. Balozi Dkt.Batilda amejionea miradi ya kimkati inayofanywa na shirika hilo kwa teknolojia ya Visual Reality.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Bi. Latifa Khamis amefurahiswa na jinsi ambavyo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeweka teknolojia ya Visual Reality ambayo inamuwezesha mtembeleaji wa banda hilo kuona picha halisi za miradi ya kimkakati unayotekelezwa na shirika hilo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news